Je Antibiotiki ( vijiuasumu) vinaweza kuzuia au kutibu COVID-19?

Hapana. Antibiotiki hazifanji kazi dhidi ya virusi,hufanya kazi ya kuuwa bakteria pekee.COVID-19 inasababishwa na kirusi, kwahiyo antibiotiki hazitafanya kazi. Hazifai kutumika kama njia ya kujikinga au kutibu COVID-19. Zitumike pale tu endapo daktari atashauri kutibu maambukizi ya bakteria.

Je kuna dawa nyingine au tiba mbadala zinazozuia COVID-19?

Wakati tiba za maghalibi, asili na za nyumbani zinaweza kuleta auheni ya dalili za COVID-19, hakuna ushahidi wahivi karibuni wa dawa zozote zinazoweza kuzuia au kutibu hili gonjwa. WHO haipendekezi tiba binafsi kwa kutumia dawa yoyote, ikiwemo antibiotiki,kama kinga na tiba ya COVID-19. Hata hivyo , kuna majaribio yanafanywa yanayotumia kuchanganya tiba asili na zile za magharibi. WHO itaendelea kutoa mrejesho wa taarifa pale punde tiba itakapo gundulika.

Kuna chanjo, dawa au tiba ya COVID-19?

Mpaka wa leo bado hakuna chanjo na dawa za kuuwa virusi inayozuia COVID-19. Japo kuwa, wale walioathirika wanapaswa kupewa uangalizi ili kupunguza dalili. Watu wenye magonjwa sugu wanapaswa kulazwa hospitali. Wagonjwa wengi wanapata ahueni kutokana na uangalizi wanaopatiwa.

Chanjo za majaribio na dawa maalumu bado zipo chini ya uchunguzi. Zimekuwa zikitumiwa kwa majaribio ya kliniki.WHO inaratibu juhudi za kutengeneza chanjo na madawa kuzuia na kutibu COVID-19.

Njia madhubuti kujikinga binafi na wengine dhidi ya COVID-19 ni kuosha mikono mara kwa mara, kujifunika kwa kiwiko au kitambaa wakati unapokohoa, na kuweka umbali wa japo mita 1 ( futi 3) na watu wanaokohoa au kupiga chafya.