Dalili za kawaida za ugonjwa wa COVID-19 ni:

  1. Homa
  2. Uchovu
  3. Kikohozi kikavu.
  • Baadhi ya wagonjwa wanaweza kupata maumivu, msuguano wa pua, kutokwa kwa majimaji puani, vodonda vya koo au kuharisha.
  • Dalili hizi huanza polepole. Baadhi ya watu wanapata maambukizi bila kuonesha dalili zozote za ugonjwa.
  • Watu wengi (takribani 80%) wanapona kutokana na ugonjwa huu bila ya matibabu maalum. Takribani katika kila watu 6 wenye ugonjwa wa COVID-19 mtu 1 huwa mgonjwa sana na kupelekea kupumua kwa shida.
  • Wazee na wale wenye shida za kimatibabu kama vile shinikizo la damu, matatizo ya moyo au ugonjwa wa kisukari wana uwezekano wa kupata ugonjwa kwa dalili mbaya.
  • Watu wenye homa, kikohozi na ugumu wa kupumua wanapaswa kupata matibabu.