Hapana. Virusi vinavyosababisha COVID-19 na vile vilivyosababisha mlipuko wa SARS mwaka 2003 vinahusiana kwa vinasaba, lakini magonjwa yanayosabishwa ni tofauti kidogo. SARS ulikua na vifo vingi lakini hali ya maambukizi ni kidogo kuliko COVID-19. Hakujatokea mlipuko wowote wa SARS duniani tangu mwaka 2003.