• Ni kawaida kuwa na huzuni, sonona, kuchanganyikiwa, kuogopa au hasira wakati wa majanga. Kuongea na watu unaowaamini husaidia. Wasiliana na marafiki na familia.
  • Kama utakaa nyumbani, dumisha mfumo wa maisha wenye afya- ikiwemo mlo bora, kulala, mazoezi na mawasiliano ya kijamii na uwapendao nyumbani na barua pepe au simu kwa familia na marafiki.
  • Usivute sigara, pombe au vilevi vingine katika kukabili hali hisia zako. Kama unahisi kuzidiwa zaidi, ongea na mtu wa afya au mshauli. Ikiwezekana weka mipango,wapi pakwenda na jinsi ya kupata huduma ya afya ya mwili na akili.
  • Pata ukweli.Kusanja taarifa ambazo zitakusaidia kwa ufasaha kujua hatari ili uweze kuchukua hatua zinazofaa, Tafuta chanzo kinachoaminika kama tovuti ya shirika la afya duniani WHO , au la ndani au shirika la afya kitaifa.
  • Zuia wasi na mvutano kwa kupunguza muda wa wewe na familia yako kuangalia au kusikiliza vyombo vya habari ambavyo unaona vinaleta huzuni.
  • Tumia ujuzi ambao umeshautumia kitambo ambao umekusaidia kupambana na magumu ya maisha na utumie ujuzi huo kukusaidia kuthibiti hisia zako katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa.

Kuwasaidia watoto katika kukabiliana na msongo wakati wa COVID-19

  • Watoto huonyesha msongo kwa njia tofauti kama vile kuwa na mashaka, kujiondoa, hasira au mvutano, kujikojolea n.k. Itikia matendo ya mwanao kwa njia chanya, sikiliza mahitaji yao na wape upendo na umakini zaidi.
  • Watoto wanahitaji upendo kwa watu wazima kipindi hiki kigumu. Wapatie muda na umakini wako zaidi. Kumbuka kuwasikiliza, kuongea kwa upole na kuwahakikishia. Ikiwezekana, tengeneza mazingira waweze kucheza na kupumzika.
  • Jaribu kuwaweka watoto karibu na wazazi na familia na acha kuwatenga mbali watoto na walezi wao. Kama utengano ukitokea (mf. Kulazwa) hakikisha kuna mawasiliano endelevu ( simu) na wape uhakika.
  • Endeleza ratiba na njia zile zile iwezekanavyo, au saidia kutengeneza mpya katika mazingira mapya, ikiwemo shule/kujifunza na kucheza katika hali ya usalama.
  • Toa ukweli kuhusu kinachoendelea, elezea kinachoendelea na wapatie taarifa sahihi ya jinsi ya kupunguza hatari ya maambukizi kupitia maneno watakayo weza kukuelewa kutokana na umri wao. Hii pia inajumlisha kuwapa taarifa kuhusu matarajio ya mbeleni (kama mmoja wa familia ataumwa na atahitaji kwenda hospitali.