Vaa barakoa kama unaumwa na dalili za COVID-19 ( hasa kikohozi) au kama unamuuguza mtu alieathirika na COVID-19.Barakoa za kutumia na kutupa zinafaa kutumika mara moja tu. Kama auhumwi au kuuguza mgonjwa basi unatumia barakoa vibaya. Kuna uhaba wa barakoa ulimwenguni, hivyo WHO inaomba zitumike kwa busara.
WHO inashauri kutumia barakoa za kiafya kuzuia matumizi yasiyo ya lazima ya rasilimali na matumizi mabaya ya barakoa.
Njia pekee ya kujilinda mwenyewe na wengine dhidi ya COVID-19 ni kuosha mikono, kufunika kwa kiwiko au kitambaa wakati unapokohoa au kupiga chafya.